10. Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme;Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.
11. Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya BWANA;Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.
12. Wafalme wakitenda yasiyo haki ni chukizo;Maana kiti cha enzi huthibitika kwa haki.
13. Midomo ya haki ni furaha ya wafalme;Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.