19. Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba;Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20. Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21. Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22. Pasipo mashauri makusudi hubatilika;Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
23. Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24. Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.