11. Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12. Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13. Moyo wa furaha huchangamsha uso;Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14. Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15. Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya;Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.