Mit. 15:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Jawabu la upole hugeuza hasira;Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

2. Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri;Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.

3. Macho ya BWANA yako kila mahali;Yakimchunguza mbaya na mwema.

4. Ulimi safi ni mti wa uzima;Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.

5. Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.

Mit. 15