1. Jawabu la upole hugeuza hasira;Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
2. Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri;Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
3. Macho ya BWANA yako kila mahali;Yakimchunguza mbaya na mwema.
4. Ulimi safi ni mti wa uzima;Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5. Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.