15. Mjinga huamini kila neno;Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.
16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.
17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.
18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.
19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.