Mit. 14:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Mjinga huamini kila neno;Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.

16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.

17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.

18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.

19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.

Mit. 14