9. Nuru ya mwenye haki yang’aa sana;Bali taa ya mtu mbaya itazimika.
10. Kiburi huleta mashindano tu;Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
11. Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka;Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.
12. Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.