7. Kuna mtu mwenye kujitajirisha, lakini hana kitu;Kuna ajifanyaye kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.
8. Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake;Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote.
9. Nuru ya mwenye haki yang’aa sana;Bali taa ya mtu mbaya itazimika.
10. Kiburi huleta mashindano tu;Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.