Mit. 13:10-13 Swahili Union Version (SUV)

10. Kiburi huleta mashindano tu;Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.

11. Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka;Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.

12. Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.

13. Kila alidharauye neno hujiletea uharibifu;Bali yeye aiogopaye amri atapewa thawabu.

Mit. 13