11. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12. Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14. Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
15. Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe;Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16. Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara;Bali mtu mwerevu husitiri aibu.