Mit. 12:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa;Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.

2. Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.

3. Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.

4. Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.

Mit. 12