18. Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;Apandaye haki ana thawabu ya hakika.
19. Haki huelekea uzima;Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.
20. Wenye kuhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.
21. Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu;Bali wazao wa wenye haki wataokoka.