Mit. 11:12-20 Swahili Union Version (SUV)

12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.

15. Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.

16. Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;Na watu wakali hushika mali siku zote.

17. Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;Aliye mkali hujisumbua mwili wake.

18. Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;Apandaye haki ana thawabu ya hakika.

19. Haki huelekea uzima;Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.

20. Wenye kuhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.

Mit. 11