Mit. 11:1-14 Swahili Union Version (SUV)

1. Mizani ya hadaa ni chukizo kwa BWANA;Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.

2. Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu;Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.

3. Ukamilifu wao wenye haki utawaongozaBali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.

4. Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;Bali haki huokoa na mauti.

5. Haki yake mtu mkamilifu itamwongoza njia yake;Bali mtu mwovu ataanguka kwa uovu wake.

6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.

7. Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea;Na matumaini ya uovu huangamia.

8. Mwenye haki huokolewa katika dhiki,Na mtu mwovu ataiingia badala yake.

9. Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;Bali wenye haki watapona kwa maarifa.

10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.

11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.

12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.

Mit. 11