7. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.
8. Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
9. Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.
10. Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
11. Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,
12. Kuchukiana huondokesha fitina;Bali kupendana husitiri makosa yote.
13. Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu;Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu.
14. Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa;Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.
15. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Uangamivu wa maskini ni umaskini wao.
16. Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima;Mazao ya wabaya huuelekea dhambi.
17. Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima;Bali yeye aachaye maonyo hukosa.
18. Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo,Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.
19. Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu;Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.
20. Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule;Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.
21. Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi;Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.
22. Baraka ya BWANA hutajirisha,Wala hachanganyi huzuni nayo.
23. Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima.
24. Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia;Na wenye haki watapewa matakwa yao.
25. Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena;Bali mwenye haki ni msingi wa milele.
26. Kama siki menoni, na kama moshi machoni,Ndivyo alivyo mtu mvivu kwao wamtumao.
27. Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu;Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.