Mit. 10:4-10 Swahili Union Version (SUV)

4. Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini;Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.

5. Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima;Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.

6. Baraka humkalia mwenye haki kichwani;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.

7. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.

8. Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

9. Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.

10. Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

Mit. 10