Mit. 10:14-19 Swahili Union Version (SUV)

14. Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa;Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.

15. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Uangamivu wa maskini ni umaskini wao.

16. Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima;Mazao ya wabaya huuelekea dhambi.

17. Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima;Bali yeye aachaye maonyo hukosa.

18. Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo,Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.

19. Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu;Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.

Mit. 10