Mik. 1:12-15 Swahili Union Version (SUV)

12. Maana akaaye Marothi ana utungu wa mema;Kwa kuwa msiba umeshuka toka kwa BWANA,Umefika mpaka lango la Yerusalemu.

13. Mfungie gari la vita farasiAliye mwepesi, ukaaye Lakishi;Alikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni;Maana makosa ya Israeli yameonekana kwako.

14. Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi ya kuagia;Nyumba za Akzibu zitakuwa kijito kidanganyacho wafalme wa Israeli.

15. Bado, ukaaye Maresha, nitakuletea yeye atakayekumiliki;Utukufu wa Israeli utafika mpaka Adulamu.

Mik. 1