Mhu. 8:5-8 Swahili Union Version (SUV)

5. Aishikaye amri hatajua neno baya;Na moyo wa mwenye hekima hujua wakati na hukumu.

6. Kwa maana kwa kila shauri kuna wakati na hukumu; kwa sababu mashaka ya mwanadamu yaliyo juu yake ni makubwa;

7. kwa kuwa hajui yatakayokuwako; kwa maana ni nani awezaye kumweleza jinsi yatakavyokuwa?

8. Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho;Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa;Wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile;Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.

Mhu. 8