1. Mainzi mafu huvundisha marhamu ya mwuza marashi;Kadhalika upumbavu haba ni mzito kuliko hekima na heshima.
2. Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume;Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto.
3. Naam, huyo mpumbavu tena, aendapo njiani, hupungukiwa na fahamu zake; hata humwambia kila mtu ya kuwa yeye ni mpumbavu.