1. Maneno ya Mhubiri, mwana wa Daudi, mfalme katika Yerusalemu
2. Mhubiri asema, Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili.
3. Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?
4. Kizazi huenda, kizazi huja; nayo dunia hudumu daima.