3. Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni.
4. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
5. Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
6. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.