Mdo 9:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni.

4. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi?

5. Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.

6. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.

Mdo 9