17. nikikuokoa na watu wako, na watu wa Mataifa, ambao nakutuma kwao;
18. uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.
19. Kwa hiyo, Ee Mfalme Agripa, sikuyaasi yale maono ya mbinguni,