Mdo 12:13-15 Swahili Union Version (SUV)

13. Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.

14. Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango.

15. Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. Wakanena, Ni malaika wake.

Mdo 12