Lk. 8:44-48 Swahili Union Version (SUV)

44. alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.

45. Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga.

46. Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.

47. Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara.

48. Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani.

Lk. 8