Lk. 4:32-35 Swahili Union Version (SUV)

32. wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa kuwa neno lake lilikuwa na uwezo.

33. Na ndani ya sinagogi mlikuwa na mtu mwenye roho ya pepo mchafu, akalia kwa sauti kuu,

34. akisema, Acha! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Nakujua u nani, Mtakatifu wa Mungu.

35. Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, mtoke. Ndipo yule pepo akamwangusha katikati, akamtoka asimdhuru neno.

Lk. 4