12. Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
13. Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.
14. Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando.
15. Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote.