Lk. 4:12-15 Swahili Union Version (SUV)

12. Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

13. Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.

14. Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando.

15. Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote.

Lk. 4