5. Wakafurahi, wakapatana naye kumpa fedha.
6. Akakubali, akatafuta nafasi ya kumsaliti kwao pasipokuwapo mkutano.
7. Ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu, ambayo ilipasa kuchinja pasaka.
8. Akawatuma Petro na Yohana, akisema, Nendeni, mkatuandalie pasaka tupate kuila.
9. Wakamwambia, Wataka tuandae wapi?