Lk. 2:26-36 Swahili Union Version (SUV)

26. Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27. Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,

28. yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29. Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako,Kwa amani, kama ulivyosema;

30. Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,

31. Uliouweka tayari machoni pa watu wote;

32. Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa,Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.

33. Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake.

34. Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa.

35. Nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.

36. Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.

Lk. 2