Lk. 2:25-31 Swahili Union Version (SUV)

25. Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.

26. Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27. Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,

28. yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29. Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako,Kwa amani, kama ulivyosema;

30. Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,

31. Uliouweka tayari machoni pa watu wote;

Lk. 2