Lk. 18:15-29 Swahili Union Version (SUV)

15. Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea.

16. Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.

17. Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.

18. Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?

19. Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.

20. Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.

21. Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu.

22. Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.

23. Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.

24. Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!

25. Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

26. Nao waliosikia walisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?

27. Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.

28. Petro akasema, Tazama, sisi tumeviacha vitu vyetu vyote na kukufuata.

29. Akawaambia, Hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya ufalme wa Mungu,

Lk. 18