8. Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;
9. nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.
10. Siku ya sabato alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo.
11. Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.
12. Yesu alipomwona alimwita, akamwambia, Mama, umefunguliwa katika udhaifu wako.