4. Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani.
5. Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu;
6. na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu.
7. Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.
8. Na mji wo wote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu;
9. waponyeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa Mungu umewakaribia.
10. Na mji wo wote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni,