1. Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
2. Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.
3. Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.
4. Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani.
5. Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu;