Lk. 1:52-56 Swahili Union Version (SUV)

52. Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi;Na wanyonge amewakweza.

53. Wenye njaa amewashibisha mema,Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.

54. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;Ili kukumbuka rehema zake;

55. Kama alivyowaambia baba zetu,Ibrahimu na uzao wake hata milele.

56. Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.

Lk. 1