Lk. 1:50-55 Swahili Union Version (SUV)

50. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizaziKwa hao wanaomcha.

51. Amefanya nguvu kwa mkono wake;Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

52. Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi;Na wanyonge amewakweza.

53. Wenye njaa amewashibisha mema,Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.

54. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;Ili kukumbuka rehema zake;

55. Kama alivyowaambia baba zetu,Ibrahimu na uzao wake hata milele.

Lk. 1