Lk. 1:40-43 Swahili Union Version (SUV)

40. akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.

41. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;

42. akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

43. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?

Lk. 1