40. akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.
41. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;
42. akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
43. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?