2. Mtwae Haruni, na wanawe pamoja naye, na yale mavazi, na mafuta ya kutia, na ng’ombe mume wa sadaka ya dhambi, na kondoo waume wawili, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu;
3. kisha ukutanishe mkutano wote hapo mlangoni pa hema ya kukutania.
4. Basi Musa akafanya kama alivyoambiwa na BWANA; na huo mkutano ulikutanishwa mlangoni pa hema ya kukutania.
5. Musa akawaambia mkutano, Neno aliloliagiza BWANA kwamba lifanywe, ni hili.