Law. 19:29-34 Swahili Union Version (SUV)

29. Usimnajisi binti yako, ili kumfanya awe kahaba; isiwe hiyo nchi kuuandama ukahaba, na nchi kujawa na uovu mkuu.

30. Zishikeni Sabato zangu, mpaheshimu patakatifu pangu; mimi ndimi BWANA.

31. Msiwaendee wenye pepo, wala wachawi; msiwatafute; ili kutiwa unajisi na wao; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

32. Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi BWANA.

33. Na mgeni akikaa pamoja nawe katika nchi yako, usimdhulumu.

34. Mgeni akaaye pamoja nawe atakuwa kama mzalia kwenu; mpende kama nafsi yako; kwa maana ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Law. 19