Law. 14:53-57 Swahili Union Version (SUV)

53. lakini ndege aliye hai atamwacha atoke mle mjini aende nyikani; ndivyo atakavyofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo nyumba; nayo itakuwa safi.

54. Hiyo ndiyo sheria ya pigo la ukoma ya kila aina, na ya kipwepwe;

55. na ya ukoma wa vazi, na ukoma wa nyumba;

56. na kivimbe, na kikoko na kipaku king’aacho;

57. ili kufunza itakapokuwa ni unajisi, na itakapokuwa ni safi; hiyo ndiyo sheria ya ukoma.

Law. 14