Law. 13:14-18 Swahili Union Version (SUV)

14. Lakini po pote itakapoonekana nyama mbichi kwake mtu huyo, atakuwa yu najisi.

15. Kuhani ataiangalia hiyo nyama mbichi, naye atasema kuwa yu najisi; ile nyama mbichi ni najisi; ni ukoma.

16. Au kama hiyo nyama mbichi iligeuka tena, na kugeuzwa kuwa nyeupe, ndipo atamwendea kuhani,

17. na huyo kuhani atamwangalia; na tazama, ikiwa hilo pigo limegeuzwa kuwa jeupe, ndipo huyo kuhani atasema kuwa yu safi huyo aliyekuwa na pigo; yeye yu safi.

18. Tena mwili wa mtu utakapokuwa na jipu katika ngozi yake, nalo limepoa,

Law. 13