Kut. 25:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. BWANA akanena na Musa, akamwambia,

2. Waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu.

3. Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii; dhahabu, na fedha, na shaba,

4. na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na nguo za kitani safi, na singa za mbuzi;

Kut. 25