26. Siku sita mtaokota; lakini siku ya saba ni Sabato, siku hiyo hakitapatikana.
27. Ikawa siku ya saba wengine wakatoka kwenda kukiokota, wasikione.
28. BWANA akamwambia Musa, Mtakataa kuyashika maagizo yangu na sheria zangu hata lini?
29. Angalieni, kwa kuwa BWANA amewapa ninyi hiyo Sabato, kwa sababu hii huwapa siku ya sita chakula cha siku mbili; kaeni kila mtu mahali pake, mtu awaye yote asiondoke mahali pake kwa siku ya saba.