Kut. 15:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na kusema,Nitamwimbia BWANA, kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.

2. BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu;Naye amekuwa wokovu wangu.Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu;Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.

3. BWANA ni mtu wa vita,BWANA ndilo jina lake.

4. Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini,Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.

Kut. 15