Kum. 7:9-11 Swahili Union Version (SUV)

9. Basi jueni ya kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu;

10. naye huwalipa wamchukiao mbele ya uso wao, kuwaangamiza. Hatakuwa mlegevu kwake yeye amchukiaye, atamlipa mbele ya uso wake.

11. Basi zishike amri, na sheria, na hukumu ninazokuamuru leo, uzitende.

Kum. 7