5. Akawa mfalme katika Yeshuruni,Walipokutanika wakuu wa watu,Makabila yote ya Israeli pamoja.
6. Reubeni na aishi, asife;Lakini watu wake na wawe wachache.
7. Na baraka ya Yuda ni hii; akasema,Isikize, Ee BWANA, sauti ya Yuda,Umlete ndani kwa watu wake;Alijitetea kwa mikono yake;Nawe utakuwa msaada juu ya adui zake.
8. Akamnena Lawi,Thumimu yako na Urimu yako vina mtakatifu wako,Uliyemjaribu huko Masa;Ukateta naye kwenye maji ya Meriba.