Kum. 33:16-27 Swahili Union Version (SUV)

16. Na kwa vitu vilivyo bora vya nchi, na kujaa kwake,Na uradhi wake aliyekaa ndani ya kile kijiti;Na ije baraka juu ya kichwa chake Yusufu,Juu ya utosi wa kichwa chake aliyetengwa na nduguze.

17. Mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe wake mume, enzi ni yake;Na pembe zake ni pembe za nyati;Kwa hizo atayasukuma mataifa yote, hata ncha za nchi;Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,Nao ni maelfu ya Manase.

18. Na Zabuloni akamnena,Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako;Na Isakari, katika hema zako.

19. Watayaita mataifa waje mlimani;Wakasongeze huko sadaka za haki;Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari,Na akiba zilizofichamana za mchangani.

20. Na Gadi akamnena,Na abarikiwe amwongezaye Gadi;Yeye hukaa kama simba mke,Hurarua mkono, naam, na utosi wa kichwa.

21. Akajichagulia sehemu ya kwanza,Kwani ndiko lilikowekwa fungu la mtoa-sheria;Akaja pamoja na wakuu wa watu,Akaitekeleza haki ya BWANA,Na hukumu zake kwa Israeli.

22. Na Dani akamnena,Dani ni mwana-simba,Arukaye kutoka Bashani.

23. Na Naftali akamnena,Ee Naftali, uliyeshiba fadhili,Uliyejawa na baraka ya BWANA;Umiliki magharibi na kusini.

24. Na Asheri akamnena,Na abarikiwe Asheri kwa watoto;Na akubaliwe katika nduguze,Na achovye mguu wake katika mafuta.

25. Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba;Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.

26. Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni,Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie.Na juu ya mawingu katika utukufu wake.

27. Mungu wa milele ndiye makazi yako,Na mikono ya milele i chini yako.Na mbele yako amemsukumia mbali adui;Akasema, Angamiza.

Kum. 33