Kum. 33:16-25 Swahili Union Version (SUV)

16. Na kwa vitu vilivyo bora vya nchi, na kujaa kwake,Na uradhi wake aliyekaa ndani ya kile kijiti;Na ije baraka juu ya kichwa chake Yusufu,Juu ya utosi wa kichwa chake aliyetengwa na nduguze.

17. Mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe wake mume, enzi ni yake;Na pembe zake ni pembe za nyati;Kwa hizo atayasukuma mataifa yote, hata ncha za nchi;Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,Nao ni maelfu ya Manase.

18. Na Zabuloni akamnena,Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako;Na Isakari, katika hema zako.

19. Watayaita mataifa waje mlimani;Wakasongeze huko sadaka za haki;Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari,Na akiba zilizofichamana za mchangani.

20. Na Gadi akamnena,Na abarikiwe amwongezaye Gadi;Yeye hukaa kama simba mke,Hurarua mkono, naam, na utosi wa kichwa.

21. Akajichagulia sehemu ya kwanza,Kwani ndiko lilikowekwa fungu la mtoa-sheria;Akaja pamoja na wakuu wa watu,Akaitekeleza haki ya BWANA,Na hukumu zake kwa Israeli.

22. Na Dani akamnena,Dani ni mwana-simba,Arukaye kutoka Bashani.

23. Na Naftali akamnena,Ee Naftali, uliyeshiba fadhili,Uliyejawa na baraka ya BWANA;Umiliki magharibi na kusini.

24. Na Asheri akamnena,Na abarikiwe Asheri kwa watoto;Na akubaliwe katika nduguze,Na achovye mguu wake katika mafuta.

25. Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba;Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.

Kum. 33