22. Msiwache, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye awapiganiaye.
23. Nikamnyenyekea BWANA wakati huo, nikamwambia,
24. Ee BWANA Mungu, umeanza kumwonyesha mtumishi wako ukubwa wako, na mkono wako wa nguvu; kwani kuna mungu gani mbinguni au duniani awezaye kufanya mfano wa kazi zako, na mfano wa matendo yako yenye nguvu?
25. Nami nakuomba nivuke, nikaione hiyo nchi nzuri iliyoko ng’ambo ya Jordani, mlima ule mzuri, na Lebanoni.