Kum. 14:8-22 Swahili Union Version (SUV)

8. na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.

9. Mtakula hawa katika wote walio majini; kila kilicho na mapezi na magamba mtakula;

10. na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.

11. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.

12. Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;

13. na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;

14. na kila kunguru kwa aina zake;

15. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;

16. na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;

17. na mwari, na nderi, na mnandi;

18. na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.

19. Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.

20. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.

21. Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye.

22. Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.

Kum. 14