12. Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;
13. na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;
14. na kila kunguru kwa aina zake;
15. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
16. na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;
17. na mwari, na nderi, na mnandi;
18. na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.
19. Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.
20. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.
21. Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye.